Hot Posts

6/recent/ticker-posts

KOCHA WA SIMBA SIO MBOVU ILA SHIDA KUSHINDANISHWA NA YANGA


Mengi yanazungumzwa kila mmoja ana hoja zake kuhusu benchi la ufundi la Simba SC lakini tunasema tunapeana nafasi kuzungumza fact


Utakuwa unafanya makosa ukiwa unamuongelea Roberto Oliveira huku ukikitazama kikosi cha Yanga SC na kuanza kufananisha uwezo wao


Ndio nawaelewa mashabiki wa Simba kuhusu muendelezo wa kikosi chao, huku nitawaelewa zaidi wale wote wanaokoa uwezo wa Kocha huyu huku wakisema hawaelewi nini plan yake


Wana Lunyasi hawajazoea kucheza nyumbani halafu waondoke vichwa chini hayo siyo mazoea yao hata kidogo


Timu inashinda mashabiki wanashikilia moyo dakika zote za mchezo, hakuna ile raha kwao huku ikiwa tofauti na Watani zao Yanga ambao wao dakika nyingi ni shangwe zaidi


Hata hivyo naamini benchi la Simba SC chini ya Kocha Mkuu Robertinho Oliviera atakuwa ameliona hilo na atalifanyia kazi kwa haraka, watu wa Simba siyo wavumilivu hua hawezi kutilia pale wanapoiona timu yake haichezi lile soka la Samba, soka safi lenye minyama nyama kwenye pitch


Hongereni wana Simba SC Kubwa timu imefuzu hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika


Hapa ni kuanza maandalizi ya kujiweka fiti kwani Octoba 20, 2023 kikosi cha Simba SC kinaenda kukabiliwa na mchezo mgumu dhidi ya Mafarao Al Ahly katika michuano mipya ya Super Cup Afrika.
 

Post a Comment

0 Comments