Hot Posts

6/recent/ticker-posts

MOROCCO WAANZA KUMUOGOPA SAMATTA, HILI NI PENGO LA KUWANYOA

 Achraf Hakimi mbele ya waandishi wa habari za michezo analitaja jina la Mbwana Samatta, anakwambia huyo ndiye mchezaji anayemjua zaidi na hakuna mwingine


Hakimi pamoja na kumjua Samatta lakini akaongezea kwamba, walaa hawamuhofii wao kama Morocco


Lakini hapa lipo jambo ndugu zangu, kitendo cha kumtaja Mbwana Samatta hiyo tu ni silaha tosha kwetu kuwabamiza hawa Morocco, naamini wataingia uwanjani akili yao yote itakuwa kwa POPA hiyo itatupa nafasi zaidi kuwatandika



Nyiee huyo Achraf Hakimi kumbukeni ni mchezaji mkubwa, mchezaji wa Dunia yaani siyo poa, Wajerumani, Wareno wote wanaijua shughuli yake huyo beki


Kucheza pale PSG tena Ligi kubwa Ulaya nchini Ufaransa siyo kitu kidogo, tunamuheshimu Hakimi lakini kesho kama Watanzania tuna jambo letu


Waliwahi kuja hapa hawa Wamorocco tukawapa chuma tatu, hii ipo kichwani kwao hadi leo kwaiyo kesho wataingia na tahadhari Kubwa wakiwa wanajua Tanzania siyo timu ya kinyonge


Mama yetu Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wetu ameshamaliza kazi ticket zote amezinunua ni sisi twendeni uwanjani

Post a Comment

0 Comments