Hot Posts

6/recent/ticker-posts

ARSENAL MSIMU HUU HAKAMATIKI KABISA


 PESA HIYOOOOO .! 


Unalipa Pauni Milioni 105 kwa mchezaji kama huyu , sio wengine mnalipa 100 hovyo hovyo tu .! 


Size ya pitch ya uwanja wa Luton ni changamoto aisee hasa kwa passing game 


✍🏻Kwa kiasi kikubwa hasa kipindi cha kwanza Gaby Jesus alikuwa anasaidia sana kwa Arsenal kusogea juu kwa 


1: Kushuka chini , kupokea mpira na kusogea nao juu ( carries ) 


2: Kushambulia space baina ya outside CBs wa Luton na wingbacks wao 


✍🏻Luton wanastahili pongezi kwa mpango wao : walitumia faida ya udogo wa pitch kwa kubana zaidi space na kutumia counter attacks plus mipira iliyokufa kupata chochote kitu . 


✍🏻Kipindi cha pili ni kama vile ilikuwa nani atafunga magoli mengi zaidi ya mwenzake , mmoja anatumia ufundi wa kuweka mali chini ( Arsenal ) mwingine anatumia ufundi wa mipira mirefu na iliyokufa ( Luton ) : mwisho Arsenal wakawapa Luton ladha ya dawa yao wenyewe . Heartbreaking 


NOTE 


1: Yule Fullback wa kushoto wa Luton : Doughty ana mwaga maji huyo 


2: Ross Barkley kama alikamia vile , kaubonda 


3: Kai Havertz anakuja bhana , kajipata tayari 


4: Bukayo Saka ni hatari , anafanya vitu kwa level ya juu sana 


5: Gaby Jesus kuna muda anakuwa Yes kuna muda No 


6: David Raya 🤔 nafikiri Ramsdale atakuwa na matumaini nafasi yake bado ipo 


7: DECLAN RICE , DECLAN UBWABWA ... PESA .! What a player . Tangu atue Arsenal sikumbuki mechi gani alicheza vibaya . Arsenal waongeze zingine £20M kwa West Ham 


8; Kafungwa Luton lakini wanachukia wengine . 😀


FT: Luton 3-4 Arsenal 



Post a Comment

0 Comments