Hot Posts

6/recent/ticker-posts

MECHI NGUMU ZAIDI BAYERN MUNICH ATUNISHIANA MISULI NA B. LEVERKUSEN


WHAT A GAME .!!! 

✍🏻Kama umekosa hii mechi daah , umekosa burudani sana mpira mwingi sana umepigika , Bayern Munich Vs Bayer Leverkusen 

✍🏻Dakika kama 10 za mwanzo , Bayern walitumia nafasi nzuri baada ya Leverkusen kusita kwenda kukabia juu maana yake Bayern wakawa na watu wengi zaidi ya Leverkusen kwenye build up ( creating overloads ) 

1: Bayern walikuwa na watu 5v3 dhidi ya Leverkusen 

2: Kwenye muundo wao wa 2-3 ( Upamecano na Kim nyuma ) huku mbele yao mstari wa Laimer Kimmich na Davies 

3: Leverkusen walikuwa wanazuia kuanzia juu na watu watatu ( Hoffman Boniface na Wirtz ) maana yake Bayern walikuwa wanatoka vizuri nyuma 

✍🏻Pale tu Leverkusen wingbacks wao ( Grimaldo na Frimpong ) walipoamua kusogea juu kusaidia pressing ndipo Leverkusen walipoingia mchezoni maana yake Frimpong na Grimaldo walikuwa wanawazuia vizuri Davies na Laimer , faida yake ? 

1: Bayern walikosa njia ya kutoka ( Outball ) ambao walikuwa ni fullbacks wao 

2: Iliwapa nafasi Xhaka na Andrich kuwa press zaidi Kimmich na Goretkza , hapo kuwalazimisha Bayern kupiga mipira mirefu ambayo ni rahisi kwa mabeki watatu wa nyuma ya Leverkusen kukabiliana nayo 

✍🏻Kuna nyakati Bayern walikubali kuingia mtego wa Leverkusen ( Baiting the press ) yani Leverkusen kama wanataka Bayern wawafanyie press ili space ifunguke nyuma ya kiungo cha Bayern na walifanikiwa maana Florian Wirtz alikuwa anapata space kubwa sana nyuma ya kiungo cha Bayern . Shida ni : Leverkusen hawakushambulia na idadi kubwa ya wachezaji 

✍🏻Kipindi cha pili , rusha shilingi yako juu ... yoyote angeweza kushinda mechi kutokana na idadi ya nafasi nzuri ambazo timu zote zilipika na umaliziaji ulikosekana au niseme tu Makipa walikuwa hodari . 

NOTE 

1: Leroy Sane kwenye ubora wake leo hatari sana 🔥

2: Ile Freekick ya Grimaldo 🔥

3: Xhaka kama hataki vile kwenye kiungo , anaachia tu mali hataki kukaa nayo 

4: King Kane hata Bundesliga anafunga tu 

5: Florian Wirtz alifanya kila kitu sahihi kuna nyakati pasi za mwisho zilimuangusha 

5: Ukiacha mara moja tu kila mmoja alipikwa lakini mechi kwa kiasi kikubwa walicheza vizuri sana : Tapsoba na Kossounou 🔥🔥

FT: Bayern 2-2 Leverkusen 



 

Post a Comment

0 Comments