Hot Posts

6/recent/ticker-posts

SIMBACELONA LEO AFRIKA ITAELEWA NI NINI KINAENDELEA TANZANIA


Ni ile mitaa ambayo Baba yako amekukataza kupita ndio mitaa ambayo SIMBARCELONA imeweka kiti na kuketi, Wahenga wasikie Mwanaume anawika kama Jogoo, mitaa ambayo haina anuani za makazi kama za Kaka Nape, ni mitaa ambayo watu wanaishi kwa TIN NUMBER inaitwa CAF CHAMPIONS LEAGUE.

Celebrating African Football! Ndio jioni ya leo sherehe za soka la Afrika zitaendelea pale Ndola, Clatous Chama ni Kamati ya Vinywaji, Kibu Denis kama Afande Muliro ni Ulinzi na Usalama, DJ weka mziki leo Playlist atasimamia DJ NGOMALUX, Hesabu Henock Inonga kama Choir Master ila sio Falsafa wa Muheza.

Waambie Watoto wadogo hizi shughuli ni za miaka mingi tangu Tajiri ni Jabir Shikamkono, enzi ambazo Dsm tunakuja kwa fuso la ndizi! Waambie Vijana hizi show za Mnyama tangu miaka hiyo Mwalimu yupo na Azimio la Arusha, Edward Sokoine ni Waziri Mkuu na Marehemu Shekilango ni Waziri wa Nchi, kabla ya B Levo na Mwijaku na Wazee wa sasa wanafuta kamasi kwa ngumi.

Jioni ya leo ni siku nyingine tena Mnyama wa nyikani anaenda kuunguruma! Aungurumapo Simba Mchezaji nani kwa sauti ya Mwanamasanja Banza Stone RIP, Simba na Ligi ya Mabingwa ni kama Dangote na Zuhura, raha ya soka la Afrika ni kama Mwanamke akiwa na dera akionesha chura, wasaa wa wababe kukaa shura na kumtazama Sunderland.

SIMBARCELONA ni kinywaji rasmi kusini mwa Jangwa la Sahara

VISIT MOROGORO🇹🇿

 

Post a Comment

0 Comments