Hot Posts

6/recent/ticker-posts

Duuuuh Kwahiyo AVIC TOWN NI BORA KULIKO UTURUKI???

🗣️Baadhi ya wadau wengi wa soka hapa nchini Tanzania walikuwa na maoni tofauti baada ya kusikia kambi ya klabu ya Yanga kwamba itakuwa Kigamboni Avic town, Watu wengi waliona kwamba Yanga haiwezi kuwa na maandalizi bora hapa Tanzania kwakua timu kama Simba kwenda Uturuki na Azam kwenda Tunisia, Ikaonekana kama klabu ya Yanga haina pesa ya kufanya maandalizi ya msimu mpya nje ya Tanzania.


🗣️Lakini mpaka sasa klabu ya Yanga imeonyesha kwamba ndani ya Tanzania unaweza ukafanya maandalizi na timu yako na ukapata ulichokuwa unahitaji kama ulikuwa na mipango mizuri na kuwa na kocha mzuri wa kuandaa timu kuelekea msimu mpya


🗣️Klabu za Simba na Azam ambazo ziliweka kambi nje ya nchi, Mpaka kwa mechi walizocheza zinaonyesha maandalizi yao hayakuwa mazuri ndio mana klabu ya Yanga katika hiki kipindi cha mechi za timu za Taifa wanahitaji kucheza mechi za kirafiki kwaajili ya kujiimalisha zaidi kwakua timu bado inaonekana inakosa muunganiko na kushindwa kucheza soka lakuvutia 


#Boiboimkali
 

Post a Comment

0 Comments