Hot Posts

6/recent/ticker-posts

HII NDIYO SIRI YA SIMBA KUSHIDA DHIDI YA PRISONS MBEYA


.

✍🏻Ndio uwanja nyasi za kijani lakini hali yake hairuhusu sana kucheza pasi za chini ( kuweka mali chini ) lakini Simba SC bado walitafuta namna ya kuwa bora uwanjani zaidi ya TZ Prisons 

✍🏻Baada ya Simba SC kufungwa goli , jinsi walivyo react ndio kocha yoyote anavyotaka 

1: Hakuna kushusha mabega chini na kujionea huruma 
2: Hakuna haja ya kupaniki 

3: Tuongeze idadi ya wachezaji wa kushambulia 

4: Tusiwape Prisons wanachokitaka ( ambacho kucheza mipira ya juu mingi ) 

5: Muundo wao wa ulinzi pale ambapo wana mpira ili kukabiliana na counter attacks ulikuwa mzuri 

6: Hakikisha unajizuia kufanya faulo zisizo za lazima kuwapa Prisons silaha wanayoipenda 

✍🏻Baada ya hapo , Prisons wakaanza kuwa watumwa , sasa ilikuwa zamu yao kuonesha wanarudi vipi mchezoni lakini kwao ilionekana plan yao ni moja tu ... weka mali ya juu kwa akina Mbangula , shinda mpira wa kwanza na ikiwezekana wa pili lakini , uzuri kwa Simba hata kama mpira wa kwanza waliukosa basi walihakikisha ule wa pili ulikuwa wao . 

✍🏻Dakika kama 20 za mwisho , Simba SC waliwapa Prisons ladha ya dawa yao , kaa nyuma na cheza kwenye counter attacks wakiamini wanao wachezaji wenye madhara ( Bocco , Chama , Saido na Kibu ) na ndio maana walikuwa wakifanya hivyo wanaonekana hatari kwa Prisons . ( Game Management ✅) 

NOTE 

1: Ile presha ya Simba SC baada ya kufungwa goli , nafikiri iliwazidi maarifa Prisons 

2: Freekick Balua Jr 🔥 hakuna namna Salim anaokoa 

3: Kennedy bhana kama vile nyota yake haing'ai lakini kila akipata nafasi ya kucheza huwa anakupa performance nzuri tu . 

4: Prisons wapo walipo kwa sasa kwenye msimamo kwasababu wanashindwa kufunga duka vizuri , makosa mengi sana na adhabu lazima ipatikane 

5: BADO HAWAJASEMA ??? 

FT: TZ Prisons 1-3 Simba SC 


 

Post a Comment

0 Comments