Hot Posts

6/recent/ticker-posts

WATANZANIA WATATU KUCHEZA UEFA NOVATUS, SAMATTA NA KASIM MANARA


Mechi za UEFA Champions League zinarejea tena wiki hii, bila shaka watanzania wengi wanasubiri kwa hamu mechi ya Shakhtar Donetsk dhidi ya FC Porto ili waweze kumshuhudia kijana wao Novatus Dismas. 

Novatus mara baada ya kumaliza mchakato wa kujiunga na Shakhtar alijiunga na Taifa Stars kwa kuwa ilikuwa ni wiki ya mechi za kimataifa. Stars ilikuwa na mchezo wa kufuzu AFCON 2023 dhidi ya Algeria. 

Mechi ya kwanza tangu ajiunge na timu hiyo ilikuwa juma lililopita ambapo alikuwa sehemu ya wachezaji wa akiba lakini hakufanikiwa kuoata nafasi ya kucheza mchezo huo.

Kwa hiyo tusubiri kuona kijana mwingine mtanzania akiingia kwenye rekodi za kucheza UEFA Champions League ambayo ni michuano mikubwa ngazi ya klabu katika bara la Ulaya.

Kumbukumbu zinaonesha kuwa Kassim Manara na Mbwana Samatta ndio watanzania waliowahi kucheza UEFA Champions League, kama Novatus atacheza basi atakuwa mtanzania wa tatu.

 

Post a Comment

0 Comments