Hot Posts

6/recent/ticker-posts

WABABE WA MADRID DERBY - ATLETICO


Vitu ambavyo nimeona leo hasa kimbinu 


✍🏻Atletico walikuwa wanatumia sana " A third man runs " na iliwapa tabu sana Real Madrid 


1: Wingbacks wao ( Molina na Lino ) pembeni ya uwanja na kunyakati walikuwa wanafanya movements nzuri sana za kuwa third man runners na mara nyingine kuwa wingers 


2: Viungo wao wa kati kulia na kushoto ( LCM + RCM ) Saul na Llorente energy yao ya kushambulia space baina ya mabeki wa kati wa Real na fullbacks wao 


✍🏻Kuna nyakati kwenye build up ya Atletico nilivutiwa na majukumu ya Hermoso ambaye yupo kati ya mabeki watatu wa nyuma wa Real , alikuwa anasogea juu kwenye kiungo kuungana na Koke kuwa namba 6 wawili . Maana yake ? 


1: Kuwazidi idadi ya viungo Real ambao walikuwa na viungo wanne ( Kroos Fede Modric na Camavinga ) wao walikuwa watano kwasababu Griezman alikuwa anashuka chini ( Griezman Saul Llorente Koke na Hermoso ) 


✍🏻Dakika 15-20 za mwisho katika kipindi cha kwanza Real Madrid walionekana kupata tiba nzuri dhidi ya 5-4-1 ya Atletico kwenye kuzuia 


1: Kutengeneza combinations pembeni ya uwanja ( Fran Garcia + Bellingham & Fede + Lucas ) 


2: Camavinga na Modric walikuwa wanashambulia space baina ya Outside CBs wa Atletico ( Savic na Hermoso ) na wingbacks wao ( Lino na Molina ) 


3. kroos kazi yake ilikuwa kudumisha umiliki wa mpira kwa Real Madrid maana yake Atletico walikuwa wanapata tabu kutoka nyuma . 


NOTE 


1: Siku zote ukiruhusu mshambuliaji kusoma namba yako ya jezi upo matatizoni ( magoli yote matatu ya Atletico yamekuwa hivyo ) 


2: Ule mkwaju wa Toni Kroos 🔥


3: Lino kila akiwa na mali , Lucas Vazquez/ Nacho wanajua shida inakuja 🔥


4: Morata hewani 🔥


5: Rodryigo alijitahidi sana kuwa busy msumbufu 🔥


FT: Atletico 3-1 Real Madrid 



Post a Comment

0 Comments