Hot Posts

6/recent/ticker-posts

UMEBURUDIKA SIMBA VS COSTAL UNION LEO?? MATOKEO YA MWISHO SIMBA 3-0 COSTAL


UMEBURUDIKA ? 

✍🏻Hii mechi kwa Coastal Union iliisha kabla ya kuchanganya vizuri , hata bila kadi nyekundu bado Simba SC walionekana imara zaidi ya Coastal katika kila kitu na kila eneo . Wamefungwa magoli matatu yenye sifa mbili tofauti 

1: Turn Over 
2: Rotations 

✍🏻Goli la kwanza Simba lilitokana na " Forced Turnover " yani kwamba Simba walilazimisha kurejesha mpira kwenye himaya yao kutoka kwa Coastal ( Lawi kufanyiwa pressing na kupoteza mali ) 

✍🏻Magoli mawili mengine ni yanahusu Rotations ya wachezaji uwanjani hasa hawa watatu ( Chama , Saido na Miquissone ) jinsi walivyokuwa wanabadilishana nafasi uwanjani ilikuwa ngumu kwa Coastal kukabaliana nao maana hawakujua nani kutoka kwao anatakiwa kukabiliana na nani kati ya hao watatu mpaka Simba kuwafungua ( Penati na win rebound Zimbwe Jr ) 

✍🏻Nafikiri baada ya kadi nyekundu , kwa Coastal ilikuwa kupunguza idadi kubwa ya magoli ya kufungwa kwa kufanya hivi vitu viwili vya msingi sana ukiwa pungufu 

1: Zuia kwa idadi kubwa ya wachezaji hasa ndani , kubali kuruhusu krosi 

2: Kaa na mpira pindi unapoupata kwa muda mrefu iwezekanavyo na kama kuupoteza basi upotezee kwenye zone ya mpinzani wako sio kwako 

✍🏻Kwa Simba SC kwao waliona ni kutunza energy yao , upo mbele magoli matatu , dhidi ya timu ambayo ipo pungufu uwanjani haina haja tena ya kukimbizana nao ili kuepusha majeraha au kutumia energy zaidi wakati kuna ratiba zingine zinakuja ( Game management ) vuta subira , pasiana sana , ikitokea nafasi ya kufunga fanya hivyo . 

NOTE 

1: Hat Trick ya Jean Baleke , hakuna raha kama ukiwa kwenye presha ya baadhi ya mashabiki halafu unakuja kupiga hat trick 🔥

2: Ajib huwa inaonekana ana enjoy sana kucheza chini ya Mwinyi Zahera 

3: Pasi za Fabrice Ngoma ni elekezi , zinamuambia mpokeaji anatakiwa kufanya nini baadae 

4: Yes , tunapenda sana kucheza kuanzia nyuma lakini muda mwingine fanya vitu rahisi ( Lameck Lawi ) alizidisha sana na credit kwa Simba kumpora mpira 

5: Get well soon Inonga 🙏🏻 

FT : Simba SC 3-0 Coastal Union 



 

Post a Comment

0 Comments