Hot Posts

6/recent/ticker-posts

MATOKEO HAYAKUPI PICHA HALISI BAYERN VS MAN U

✍🏻Mtu akiona matokeo anaweza kuhisi mechi ilikuwa tight sana lakini ni Bayern ambao wakiamua kufunga basi unaona goli lileeee linakuja . United wakifunga basi Bayern kama vile wanasema " tunakuja kufunga goli letu tena " BANG .! 


✍🏻United walianza mchezo vizuri jinsi walivyokuwa wana press na kuwalazimisha Bayern kupoteza mipira hasa pale walipokuwa wanataka kutoka nyuma 


1: Bayern walikuwa wanafanya build up na 2-3 ( Upamecano na Kim ) nyuma na mstari wa Laimer Kimmich na Davies 


2: Lakini United walikuwa wanafanya pressing kwa 4-1-4-1 Hojlund anafunga njia ya pasi kwa Kimmich huku Rashy na Pellistri kwa Fullbacks wote wa Bayern : Bruno na Eriksen wanafunga njia za pasi zinazopita kwenye halfspaces zote mbili kwasababu ya Musiala na Goretzka . 


✍🏻Bayern baada ya kutulia na kuanza kupasia mpira vizuri , ndio shida ilipoanza kwa United 


1: Musiala anakuwa maeneo ambayo anajua Casemiro na Eriksen hawawezi kufika na anajua akishapata mpira ni rahisi kupita katikati yao 


2: Kane anashuka chini kidogo ili kufanya kazi ya Lisandro na Lindelof kuwa ngumu , kwasababu wakimfuata wanaacha space nyuma yao kwa Sane na Gnabry kuishambulia , wasipomfuata anapokea mpira na kupiga pasi kwa wingers wake 


✍🏻Aina ya magoli ambayo United wanaruhusu yanafanana sana msimu huu 


1: Goli la pili dhidi ya Spurs 

2: Goli la Martin Odegaard 

3: Magoli yote ya Brighton 

4: Goli la Gnabry 


Yanafanana nini ? United wanashida sana ya kukimbia na runners wa timu pinzani ( tracking runners ) , cutbacks zinawafunga sana United msimu huu na timu zinajua hilo . Casemiro na Eriksen pamoja kwenye kiungo bila mpira ? 🤔🤔


NOTE 


1: Jamal Musiala kawapika sana viungo wa United 


2: Kimmich muda wote anapicha kichwani kwake nini kinaendelea na nini afanye 


3: Bayern bila mpira wanaacha space nyingi sana ni wewe tu kuwapa adhabu kama unataka 


4: Goli la nne la Bayern , pasi , movement na finishing 🔥


5: Andre Onana wakati anaopitia sasa hivi 🤔


6: Man United katika mechi 5 zilizopita wameruhusu magoli 14 🤔


7: Kufunga magoli 3 ugenini na bado hujashinda mechi 😭


FT: Bayern 4-3 Man United 



Post a Comment

0 Comments