Hot Posts

6/recent/ticker-posts

KOCHA WA YANGA AWEKA MSISITIZO MKALI! SISI TUNATAKA KUCHEZA MAKUNDI HADI KUFUZU


Tupo kwenye hatua ya mwisho, tuna dakika 90 za kucheza ili kufikia lengo la kucheza hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, maandalizi yapo vizuri tulikuwa na muda wa kutosha kujiandaa.


Miongoni mwa vitu vilivyonihamasisha kuja Yanga ni pamoja na kucheza Ligi ya Mabingwa Afrika , nafikiri ni mashindano bora kwenye bara hili lakini pia nafikiri imepita miaka 25 tangu klabu hii icheze hatua ya makundi ya mashindano haya.


Kesho ni mchezo mwingine mpya, tutacheza bila kufikiria matokeo ya Kigali, Rwanda, tutacheza kama matokeo ni 0-0. Tumefanya kazi kwa bidii na tunasubiri kesho kuonesha mchezo mzuri na kuwapa furaha wananchi. 


- Miguel Gamondi, Kocha Mkuu Yanga.
 

Post a Comment

0 Comments