Hot Posts

6/recent/ticker-posts

LIVERPOOL WATUMA SALAMU NZITO KWA KILA ANAYEWADHARAU


Hii ndio Ligi kuu ya soka nchini England . Just imagine being us ... just imagine it . Pungufu uwanjani tangu dakika ya 28 lakini Liverpool wamecheza kama wapo 15 uwanjani 


1: Nidhamu ya mchezo 

2: Kujipanga vizuri uwanjani 

3: Ufundi 

4: Matamanio ya kupambana 

5: Passing 

6: Hakuna mvivu uwanjani 

7: Ukatili mbele ya goli 


This is Liverpool brother and sisters 


✍🏻Kipindi cha kwanza unaangalia hii mechi ina kila kitu unachotaka kutoka kwa team ambazo zipo serious na kazi zao . Pressing ya hali ya juu, pasi za umakini sana , kuwania mpira , kasi ya mchezo na wachezaji wenyewe . 


✍🏻Baada ya kadi nyekundu kwangu mimi hapo ndio mechi ilianza rasmi kwa timu zote mbili kivipi ? 


✍🏻Klopp akaihamisha timu yake kuwa 4-4-1 bila mpira ( Salah pekee mbele ) huku mstari wa wachezaji wanne kati Elliot Szobo Jota Mac Allister kabla ya Darwin kuingia dimbani lakini bado muudo ukawa ule ule ulibadilika wakiwa na mpira tu 


✍🏻Wakiwa na mali Liverpool wanakuwa 2-4-3 ( nyuma Jarell na Gomez ) then TAA , Elliot Szobo na Robbo na mbele Jota Salah na Darwin 


✍🏻Newcastle walijipiga risasi mguuni 


1: Walianza kucheza na hisia sana badala ya kutumia akili na utulivu na hiyo kutokana na mashabiki wao 


2: Wakaanza kulazimisha kwenda mbele haraka kwa pasi nyingi za kwenda mbele badala ya kumiliki mpira na kuwafanya Liverpool wautafute 


3: Pembeni ndio ilikuwa suluhisho zuri kwao ili kuwafanya Liverpool kuzuia eneo kubwa la uwanja kwa kuwatumia Almiron na Barnes badala yake waliendelea kulazimisha kupita katikati. 


4: Unawapa pongezi kubwa Liverpool kwa uzuiaji wao licha ya kuwa pungufu . 


NOTE: 


1: Mechi ya pili Liverpool wanacheza pungufu na bado wanashinda mechi 🔥


2: TAA kosa la pili mfululizo la TAA na anaadhibiwa 


3: Gordon leo alimpika sana TAA 🔥


4: Sidhani kama kunatakiwa kuwe na mjadala kuhusu ALISSON BECKER . kipa bora Duniani full stop 🔥


5: DARWIN NUNEZ nafasi mbili kamba mbili : Clinical , ruthless, lethal 🔥🔥


6: KAMA NEWCASTLE WAMEONEWA LETA TIMU YAKO TENA LIVERPOOL WAKIWA PUNGUFU


FT: Newcastle 1-2 Liverpool

Post a Comment

0 Comments