Hot Posts

6/recent/ticker-posts

NIWAKUTE WACHEZAJI WOTE KAMBINI - BENCHIKHA

 



Baada ya mechi ya jana dhidi ya Asec Mimosas ya Ivory Coast, kikosi cha Simba kimepewa mapumziko ya siku moja na kesho kitarejea mazoezini huku kocha mkuu mpya wa timu hiyo, Abdelhak Benchikha akianza mikwara kwa kuwataka mastaa wote wa timu hiyo kambini, ili aanze mambo.


Benchika anakuchukua nafasi ya Mbrazil, Roberto Oliveira ‘Robertinho’ aliyefutwa kazi baada ya kichapo cha 5-1 ilichopata timu hiyo mbele ya Yanga, alitambulisha Ijumaa usiku, akiwa kwao Algeria na jana Jumamosi alianza safari ya kuja Bongo kabla ya kesho Jumatatu ataanza rasmi kazi ndani ya kikosi hicho.


Gazeti la Mwanaspoti limebahatika kuzungumza na kocha huyo kwa njia ya simu akiwa kwao Algeria amesema 


“Naijua Simba ni timu nzuri na imekuwa na ushindani mkubwa katika bara hili la Afrika, nina furaha kujiunga nao. Kwa sasa siwezi kusema chochote kuhusu mipango yangu binafsi, naenda kutimiza mipango ya timu kutokana na makubaliano yetu,” amesema Benchikha na kuongeza;


“Kitu cha kwanza nitakachofanya ni kukutana na wachezaji wote kambini, nataka nionane na kila mmoja na kutambua uwezo wake na baada ya hapo nitaanza kutengeneza timu nikiendeleza nilipoikuta.”


Benchikha ataanza kuiongoza Simba kwenye mechi ya michuano ya CAF, itakayopigwa Desemba 2 ugenini dhidi ya Jwaneng Galaxy ya Botswana, ukiwa ni mchezo wa pili kwenye kundi la timu hizo lenye Wydad Casablanca ya Morocco.

Post a Comment

0 Comments