Hekaya za Kombo
Kupata Unga wa Ugali Nusu Kilo ni Kazi.
Mashabiki wenye hisia hasi wameamua kujidanya eti Simba wamecheza vizuri na wachambuzi waliowekewa vibuyu vya asali mdomoni wanasema Simba wamefanikiwa sana kwenye mchezo dhidi ya Al Ahly na hadithi za vijiwe vya waponda kokoto kila neno ilibaki kidogo tu tupate unga wa ugali nusu kilo.Kuna tatizo kubwa sana la kuvuka mstari unaotenganisha giza na mwanga.
Kwangu mimi Simba hawakucheza vizuri ndio maana hawakufanikiwa kupata hela ya kununua unga wa ugali nusu kilo kwenye michezo yote miwili kwasababu dunia inasumbulia na ugonjwa wa ukimwi pamoja ugonjwa wa Simba kuruhusu magoli kirahisi.inawezekana haya ni maneno ambayo hayana ukweli kabisa lakini uongo unaosemwa kuhusu Simba kuganda kwenye matope ya robo fainali ni ukweli ukweli.
Sijawahi kumsifia Baba ambaye ameshindwa kununua unga wa ugali nusu kilo kwa ajili ya familia kwa miaka mingi,kwangu huyu sio tu Baba mzembe isipokuwa ana matatizo ya kufikiri sahihi,Kwani tukimchukua huyu Baba tukampa jina la Simba na kisha kumwambia ukiongeza ubora kichwani hata unga kilo moja unaweza kununua sidhani kama ni dhambi au wema utakuwa umesababisha kifo,Basi Enyi watu wanywa damu eleweni bado Simba anatambaa taratibu sana kwenye tope la robo fainali.
If truth shall kill them,let them die
0 Comments