Hot Posts

6/recent/ticker-posts

CHAMA WA SIMBA NI ZAIDI YA MCHEZAJI TANZANIA


Ndio nimetoka kituo cha kati cha Polisi muda huu, Kijana wangu alikuwa rumande na shitaka lake lilikuwa dhidi ya Jamhuri, nimesaka Mawakili wa maana twende kwenye mahakama ya soka maana ni nusu twende Kisongo, Segerea, Rwanda Nzovwe ama Keko. 

Kesi yake ya kwanza ni raia wa kigeni ambaye ana matumizi mabaya ya passport yake, ameingia kama Mzambia lakini jina lake halisi sio CLATOUS CHAMA bali CLAUTINHO CHOTAES CHAMA GAUCHO ni Mbrazil kutoka kitongoji cha Mogi Da Cruzes, Sao Paulo kwa Walevi wa soka.

Kosa lake la pili ni kuleta usumbufu kwa Askari Magereza jana na kuwanyima uhuru wa kutimiza majukumu yao, aliamua Afande Salum Kimenya akimbie vipi, aliamuru Afande Jamal Masenga akae wapi na wakati gani na kwa dhumuni gani, hii ni kero kwa Jamhuri na Wizara ya mambo ya ndani ya soka imeagiza arudishwe kwao. 

Tupo nje kwa dhamana ya goli la kwanza, alipouchukua mpira katikati akichafua uwanja na sio kuchafua hali ya hewa kama Dada Mange, alishuka chini kuchukua mali na sio chumvini, false pass kisha akaondoka, akazikanyaga nyasi za sokoni na sio mafuta ya Mwamposa, one touch na akili kubwa kwenye sehemu ndogo kama kikombe cha kahawa. 

Faili lake ni namba 17/03/01 SIMBA na lipo chini ya Inspekta wa Police, Robertinho! Nimewaambia ni uhakika nashinda hii kesi kama mkeka wa ina shaka kabisa kwakuwa Bookmakers wa soka wanaitaka burudani hii iendelee pale Singida, kuna warembo na wanastahili Joga Bonito. 

The best ever to do it! Na kesho Profesa Mkenda apitishe rasmi kuwa hii ni topic huko mashuleni, kuna CRDB mbili ya kwanza ni CLATOUS REJUVENATED DEAR BROTHERS yeye ndio nguvu mpya kwenye mfumo wa Simba! Na CRDB ya pili ni Benki bora nchini 

Introduction to Clatous Chama, thats it! Thats the post! Ladies and Gentlemen! 
MANAGER. 

VISIT MOROGORO🇹🇿

 

Post a Comment

0 Comments