Hot Posts

6/recent/ticker-posts

YANGA GARI LIMEWAKA RASMI KUELEKEA UBINGWA 2023/24

 


YANGA 5-0 KMC, Champion ameanza kwenye main card baada ya mapambano ya utangulizi, baada ya Karim Mandonga fixtures ni wasaa ukafika wa kumtazama Champion in a bigger picture, walisema presha huleta changamoto ila Wananchi wakasema dhahabu safi huoshwa kwa moto, mpira mzuri mithili ya mashairi ya Mrisho Mpoto. 

 tuliwaita Mabingwa wa Kijani, moto mkali nyikani na pass zisizo mzani, mpira unatembea sio utani, msako wa kumsaka nyani unaohitaji maandishi kama Robert Shabaan, namba mbili hakuna anayemmiss Djuma Shaban! Ukisikia Koh Koh kuna Yao Yao. 


Captain Shark, Dickson with the job, bega na usinga, anacheza kama anaringa! Ujumbe kwa Admn aliyemtoa kwenye group, ameunda group jipya na anatype ujumbe wake! Goli lake la kwanza kwenye ligi, mechi yake ya kwanza kwenye ligi na ameanza ligi, tano mgongoni na tano ubaoni. 


Khalid Chukuchuku na KMC kesho kwenye kikao cha baraza la Madiwani Manispaa ya Kinondoni wataingia na jina la Mudathir Abbas, kwenye kero zote za muungano zilizopungua basi huyu Mudathir ndio kero pekee iliyosalia, amekwepa kodi mbele ya Halmashauri, amempa ugomvi Golikipa kuwa ni matumizi mabaya ya kodi, ripoti kwa CAG na hesabu za Kinondoni ni yeye ameziharibu, so good to be true. 


Step in as it is! Stephen Aziz Ki, pasi na Kiki kama King Kikii anauwasha tangu King Ki ahamie Si! As cool as you like, anatuambia Hamisa anafananaje mbele ya Rick Ross, anatuambia Wema anafananaje mbele ya Whozhu Dingoo, simply ni Mwanasoka aliyeamua kuufanya uwanja wa Chamazi kama mazoezini, Matajiri wamenuna walinunua bodi wakaacha Engine pale. 


Haters say Mwandishi kapewa laptop lakini unaachaje kuandika huu mpira heading to the top, Garmondi na energy kama Jurgen Klopp! Msimamo mliscreenshot? Maana ni muda wa kupost na kucrop, tuanze kuchungilia juu uwe mrefu kama Crouch, imara sana hii haipendwi sana hii Yanga Afrika, DJ washa Spika. 


They make it rain kama T- Pain, wanaogopesha use your brain! Machampion wameianza Ligi, zimetolewa verse nyingi wamekuja na chorus, they are the famous, welcome to the Premier League Baby! 


Mwandishi anatumika na amepewa ticket, I expect the chorus! Am out😀



VISIT MOROGORO🇹🇿

Post a Comment

0 Comments