YANGA AFRIKA, wakati Paula wa Majani yupo kwa Marioo basi Yanga Afrika mbele ya kioo uwanjani wakifanya wanachoweza kukifanya wakati wote, wanaendeleza Ufalme wao utatoka madarakani hata kama hutaki kama Milton Obote.
Soka linapigwa kubwa kama umeme wa Kidatu, Stephen Aziz Ki uliza kiatu! Kouassi Yao Yao anateleza kuliko Binti wa Kiyao, kama ulikuwa na makala yoyote tofauti basi irejeshe stoo! Try Again later.
Wakati Mheshimiwa Nape wa Mtama anazindua huduma ya 5G tayari Professor Gamondi amefunga minara mara ta
na mtandao unasoma tano, burudani yes! Soka zuri kama sauti ya Mama Sabrah Machano.
Another one kwa sauti ya DJ Khalid, siku nyingine tena ya Mkaidi haifaidi mpaka siku ya Eid, Hersi wa Kinondoni anatrend mbele ya Chino, vurugu kama Mtoto Eid! Djuma kaondoka kuna swali? Bangala hayupo haya Imaam kapata kwenye membar tuanze kuswali.
Fiston Mayele ameondoka, lakini ni kama Imaam kudhini nje ya ndoa Wananchi hawakukimbia Msikiti, ni kama Padre kulala na Sister haibadili Ukatoliki! Wananchi hawataki maua wanataka wapewe kiti wakae juu wawike kama Jogoo.
0 Comments