Hot Posts

6/recent/ticker-posts

ALIKAMWE NA AHMED ALLY WAPEWE MAUA YAO! HAKIKA VIJANA WANAWEZA

 


Ni vijana wadogo wenye kuijua vyema kazi zao


Afisa habari wa Yanga SC, Ally Kamwe na nduguye Ahmed Ally ambaye yeye ni Mkuu wa idara ya habari na mawasiliano Simba SC


Wikiendi ijayo timu zao kwa nyakati tofauti zitaingia kwenye pilka pilka tena ya michuano ya kimataifa Klabu Bingwa Afrika hatua ya makundi


Yanga SC wao watakuwa nchini Algeria dhidi ya CR Belouizdad huku Mnyama Simba SC wao watavaana na ASEC Mimosas ya Ivory coast


Napenda namna wanavyoifanya kazi yao kwani kila mmoja amechagua njia yake


Kamwe amechagua kuwa mbunifu zaidi kwa kuleta matukio mbalimbali na imeingia kweli mjini huku Ahmed Ally yeye na KISPIKA cha Mtaa


Yale magoli 5 yanakaa pembeni sasa ni kupambania klabu kwenye engo nyingine, huku kunatafutwa heshima na pesa zaidi


Nitaendelea kuwaombea afya njema na Uhai zaidi kwani kufanya vizuri zaidi hapo mlipo kunatufungulia njia na kuaminiwa sisi vijana kwamba tukiaminiwa basi inawezekana

Post a Comment

0 Comments