Hot Posts

6/recent/ticker-posts

HII KALI SANA, MBONA SIMBA MNASIRI SANA JUU YA MO DEWJI NA MANGUNGU

 



MKANGAFU: Umewahi Kunywa Ulanzi uliolala zaidi ya siku 2 ? Hapa ndugu zangu Makete, Lupila, Kidingili, Igumbilo ,Sunji na Lupalilo na Maeneo ya Jirani watakuwa wanaelewa sana,

OK NAANZA HAPA: Hakuna Mtanzania yoyote ambaye yupo Nje ya Uongozi wa klab ya Simba aliyejua kuwa Raisi wa Heshma wa klab ya Simba kwasasa ndiye Mwenyekiti wa klab hiyo 🙊, Inawezekana Mzee Mangungu akawa amestaafishwa ghafla (SOMJO SOMJO TU),

NYIE HII KALI SANA, Yaani kuna Mwenye kiti wa kuiongoza Simba Sc kwenye Michezo ya ligi ambaye ni mzee Mangungu na Kuna Mwenyekiti wa kuiongoza Simba Sc kimataifa yaani mbele ya Wageni Rasmi ambaye ni Mo dewji, (CHANGA LA MACHO),

Nilisoma Picha flani hivi wakati Patrice Motsepe akimtambulisha Mo Dewji kwa nafasi ya Uenyekiti , Mo aliinua macho kisha akawaangalia wana Simba kiuoga kisha akapiga makofi na akainama na Aliketi samba samba na Mwenyekiti wa FIFA Gian Inflantino (SHAME),

Dah Nawaza kwa sauti !!! Je Try Again na Mangungu walikuwa wapi ? 

Bado natafuta Picha na ntatoa zawadi kwa Mwenye Picha ya Mzee Mangungu akiwa amepiga Picha na Gian Inflantino, Arsene Wenger ama Collina tu,

Achana na Picha za Asha Mwalala na Mwanahamisi Gaucho kupiga wakiwa na Arsene Wenger na Viongozi wengine hizo tumeziona natafuta za Mzee Mangungu ambaye tuna aminishwa ndio Mwenyekiti wa klab ya Simba Wakati ni Uongo Mtupu,

Nitumie picha hiyo ya Mangungu inbox kwangu akiwa na Suti yake huku Pembeni yake kuna Inflantino ama Motsepe,

Nilivhogundua Simba Sc haihitaji Viongozi wasomi bali inahitaji Viongozi wa Ndio mzee, Tafsiri halisi ni tukio hili,

USICHEKE: KWANI MZEE MANGUNGU KABILA GANI ?

OK Ndugu zangu Wangoni kuna Pombe inaitwa MYAKAYA ETI ?

 NAAMBIWA WANAKUNYWA SANA WAFANYAKAZI WA SERIKALINI ? Kwa maana unakunywa Ijumaa ila utaanza kulewa Jumamosi ? 



Post a Comment

0 Comments