Hot Posts

6/recent/ticker-posts

TRIP SHAMBA TRIP GEREJI

 

✍🏻Unawapa credit kubwa sana Palace jinsi walivyokuwa wabapambana kupata ambacho walikuwa wamekifuata pale Old Trafford 

1: Zuia kwa idadi kubwa ya wachezaji bila mpira katika 5-4-1 

2: Achana na kuwa press Man United , bali mpira ukipotea rudi nyuma na funga space katikati ya uwanja waache pembeni wapige krosi 

3: Ukipata mali hakuna kubutua , unawatumia Mateta kukaa nao , Ayew kutembea nao pembeni na Eze kutembea nao nyuma ya kiungo cha United 

4: Mwisho Sam Johnstone fanya kazi yako golini . Easy point tatu wanarudi nazo London ( Nyie bakini kushinda mechi ya Carabao Cup ) 

✍🏻Man United sijui unaanzia wapi ? 

1: Chaos football . Hakuna utulivu , kila kitu kinafanywa haraka haraka . 

2: Decision making : Sehemu ya kucheza mpira rahisi , wanaufanya mgumu . Pasi rahisi , inaongezewa ugumu 

3: Casemiro , Amrabat zinachezwa rafu ambazo hazina ulazima kabisa kuwapa faida Palace pale ambapo nawataka kupumua . 

NOTE 

1: Kwani United wanacheza soka la namna gani ?? ETH anahitaji kujibu hili pia ( ni muda wa kutoka kwenye kichaka cha Glazers , inajulikana tatizo sugu lakini na yeye ana mzigo wake wa lawama . 

2: Lile goli la Andersen utasema kafunga Zidane 🔥

3: Ila Rashford ? 🤔🤔🤔

4: Kafundishwa kwenye academy ya United , katikati ya wiki kapigwa chuma 3 leo kasema hampati kitu . Saves mbili nzuri ( Sam Johnstone ) 

5: Mechi 7 za EPL na tayari United kafungwa 4 

FT: United 0-1 Palace 


Wolves kwani naye kafanyaje huko ?? Nyie hii ligi hii daah 😀😀😀😀

 

Post a Comment

0 Comments