Cristiano Ronaldo aliwaambia Real Madrid 2016 kuwa sisaini mkataba mpya bila ongezeko la asilimia ya haki za picha zangu, nataka 60-40, Real Madrid wakajizungusha sana mwishowe wakaja mezani wakakubaliana na anachotaka Mtoto wa Ureno.
David Beckham aliwaambia Man United sitosaini mkataba mpya bila kipengele cha haki za picha zangu hiyo ni 2002, United wakazungusha sana sketi na Mwanaume akaamsha zake kama utani, hivyo ndivyo Wachezaji wakubwa hufanya kwakuwa wanaijua kazi.
Mchezaji wangu, Kijana wangu ambaye Watanzania wanamtambua kama Mchezaji bora wa muda wote wengine kwa kukiri hadharani ama Msalani wakiwa wanaoga wanakubali kuwa huyu ndie GOAT wa soka la Tanzania, ana haki zote za maslahi mazuri kwakuwa hakuna anayeweza kufanya anachofanya.
Nilienda Kaskazini mwa Afrika walimtaka Kijana nikawaachia flash mezani wamtazame mimi nikaaga kwenda kunywa chai, baada ya dakika tatu walinitafuta kama Mwizi wakitaka tusaini, ila kwa heshima ya Profesa Janabi aliyeniambia Chama tangu aje wameshuhudia wagonjwa wa moyo kupungua basi nikaona abaki Tanzania.
CAF Certified Baller! Football Maestro ambaye ukitazama orodha ya Wafungaji bora wa muda wote wa CAF yupo kwenye 10 Bora! Sijui Watoto wadogo mnapata wapi jeuri za kusema anaperform mechi ndogo tu! Nendeni Google ndie Kiungo pekee kwenye orodha.
Mimi ndio Meneja pekee mwenye uhakika wa biashara yangu hapa Afrika Mashariki na kati! Hizi ndio shughuli zetu, mpeleke uwanja wowote, sehemu yoyote na shughuli zozote hizi ndio kazi zake.
Naituma hii clip Somalia, Kongo hadi Sudan! Wanamgambo wataweka silaha chini kutazama kazi ya sanaa inayotembea, Lucky Dube aliyeacha Guitar na kuamua kucheza soka! Mwalimu Nyerere aliyeacha siasa na kuzaliwa upya kwenye soka! Hahitaji promo za Wachambuzi huyu, Meneja anatosha sana! Situmi clip za tobo wala assists maana tunazo sana, zinawekwa kamba tu😀
MENEJA.
0 Comments